SABABU

"Nilikua katika umaskini na ninajua kwamba elimu ndiyo njia pekee ya kuondoka kwenye umaskini. ”

Fons Maex, MWANZILISHI wa kampuni ya Kim’s ChocOLATES

Fons Maex alikwenda Tanzania kuwatembelea wakulima wa kakao kwa mara ya kwanza mwaka 2010. Aliona wakulima, watoto na jamii nzima wakiwa katika shida kubwa. Hali ya hewa nchini Tanzania inafaa kwa kilimo cha kakao lakini wakulima wanakabiliwa na changamoto nyingi kwa sababu ya miti ya zamani na ukosefu wa elimu.

Fons alitaka kusaidia kwa namna fulani. Njia pekee ya kuondoa umaskini ni elimu, kwa hivyo hatua ya kwanza ilikuwa kutekeleza miundombinu dhaifu ya elimu katika kanda.

MWANZONI

Wakati Fons aliporudi nchini Ubelgiji
alitoa msaada wa €5,000
kwa shule kununua vitabu vya
kiada 2,000

Lakini hii ilikuwa mwanzo tu ...

HALI

1,900 vyumba vya madarasa vinavyohitaji kakujengwa au kukarabatiwa
430,000 vitabu vya kiada vinavyohitajika
65,000 watoto watakaofaidika
kutokana na mradi huu
20-25,000 familia zinazotegemea
zao la kakao mkoani
Mbeya, Tanzania

Mazoea ya kazi kwenye mashamba ya kakao ni suala, na watoto wengi wanashiriki katika kazi za kilimo zilizo hatari au wanafanya kazi badala ya kuhudhuria shule.

Wakulima
wanapata
chini ya dola
za Marekani
1 kwa siku Mashamba madogo
Uzalishaji mdogo sana
Miti ya kakao kuzeeka

KILE TUMEFANYA HADI SASA

Kukamilisha na kukarabati...

hadi
mwaka
2021
2022
1496
213

...vyumba vya madarasa

174
41

...ofisi za walimu

111
11

...ofisi za walimu wakuu

* Takwimu hizi zinaonyesha majengo yaliyozinduliwa tu

SHUGHULI ZINGINE

Imekamilika
MAKTABA
VYOO
HIFADHI
MAABARA

121
Tumekamilisha VILIMO
2 VYA MAJI
5 inajengwa

3 MABWENI ya
wasichana 240 yalikamilishwa
Bado kununua
120,000
vitabu

KUCHANGISHA FEDHA

Sisi huweka bei moja kwenye utozaji wa
kodi ambayo tunaweka kwa kila tani ya maharagwe
ya kakao inayonunuliwa kwa niaba yetu.



Tangu 2015, tumechanga takriban 5.700.000€

Kim's Chocolates ni sehemu ya Shirika lisilo la Kiserikali la Cocoa Horizons kupitia michango ambayo Kim hulipa kwa Barry Callebaut. Kakao tunayolipa michango haitoki Tanzania pekee bali hata mikoa mingine duniani. Kim's Chocolates imechagua kuwekeza michango yake kwa Cocoa yetu kwa Shools nchini Tanzania pekee.

WASHIRIKA WENGINE

Viwanda vya ndani:

Tunaweza kununua nyenzo zetu za ujenzi kwa bei rahisi sana
- Saruji: Cement Mbeya (LafargeHolcim) - Mbeya
- Mabati/mapaa na chuma za rebar: Alaf - Dar es Salaam
- Rangi: Berger Paint International - Dar es Salaam
- Mbao/milango na madirisha: Sao Hills - Mafinga (kutoka asili endelevu tu)

WANAVIJIJI hufyatua matofali na wao hutoa wafanyakazi Hivi karibuni tutabadili kwa SSB (stabilized soil block), matofali yanayofungamana ya udongo saruji, ambayo pia ni endelevu zaidi.
MAMLAKA Kwa sasa msaada wao ni maadili tu kutokana na ukosefu wa rasilimali.

JUU YA HAYO

Kwa sababu umaskini ni mojawapo ya sababu kuu ambazo watoto hawaendi shule, kampuni ya Kim’s Chocolates na washirika wake pia wanalenga kuongeza uzalishaji wa zao la kokoa kwa njia ya:

Tumezambaza
miche mipya ya kakao

350,000 na kuondokana na miti ya zamani yenye uzalishaji wa chini
Kila mwaka tunatoa mafunzo kwa wakulima wa kakao katika kupogoa, matumizi bora ya pembejeo, magonjwa na jinsi ya kuzuia/kuponya magonjwa hayo, uchachishaji, kuzuia ajira ya watoto, n.k.

Mambo mengine ambayo yanahitaji kufanywa katika eneo hili:

Ukosefu wa maji safi husababisha magonjwa mengi (ugonjwa wa kuhara damu, kipindupindu, ...). Vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano vilikuwa 4.87% mwaka 2015.

Tunatarajia:

  • Kuchimba visima vya maji katika shule zote
  • Kuweka mitambo ya kusukuma maji kwenye majengo ya shule
  • Kujenga vyoo vipya vya kisasa vya maji na vilivyo na mabeseni ya kunawia mikono
  • Kujenga bafu la umma ambalo wakati wa mchana linaweza kutumiwa na wanafunzi na baada ya shule kutumiwa na watu kutoka vijijini
  • Kujenga nyumba mpya za walimu (zenye mabomba ya maji, vyoo vya ndani) ili kuwavutia watu kufundisha vijijini.

Katika vijijini Afrika, hakuna umeme, takriban watu milioni 250 hutumia mafuta ya taa kupata mwangaza katika nyumba zao

Mafuta ya taa husababisha:

  • magonjwa mengi ya macho, magonjwa ya mapafu, kuchomeka vibaya
  • moto katika kaya

Familia hazina uwezo wa kulipa paneli ndogo za jua, lakini tunaweza kuwapa paneli hizi kupitia mikopo midogo midogo. Kila wiki wangetulipa TZS 5,000, pesa ambazo wangetumia kununua mafuta ya taa.

UDHAMINI WA MASHIRIKA

Mbali na kampuni ya Kim’s Chocolates na kampuni ya Biolands kuna wadhamini wengine wengi waliojiandikisha nasi. Ikiwa ungependa kujiunga na kuwa mwanachama wa umati huu wa wafidhiliwa unaweza kutuandikia barua pepe kupitia anwani fons.maex@kimchoc.be

Cocoa for Schools imepokea michango kutoka kwa watu binafsi na kutoka kwa wafanyakazi wa kampuni ya Kim’s Chocolates. Michango mikubwa ya ukarimu ilitoka kwa Johan Dekempe (Ubelgiji), Peter & Gertie Miehle (Ujerumani), Désiré Collen (Ubelgiji), Louise Tsang (Hong Kong) na Petra Wong (Hong Kong).

WATU HUSIKA WANAOTEKELEZA MRADI HUU

  • Fons Maex

    Fons ni mwanzilishi wa Kampuni ya Kim’s Chocolates. Alianza programu ya"Cocoa for Schools". Fons hufuatilia majengo yote ya shule na husafiri Tanzania mara kwa mara ambako anasimamia miradi yetu.

  • Michael Molesi

    Mhandisi wa ujenzi

  • Emmanuel Mwacha

    Msimamizi wa mradi

  • Zacharia Kahimba

    Msimamizi wa shamba

Bonyeza hapa kurudi kwenye ukurasa wa mwanzo.